Umoja wa Watanzania Canton Ohio Tanzanian Association of Canton, Ohio TAC.
Ni umoja ambao uliasisiwa au ulianzishwa na waasisi wa Umoja huu na kuweza kufikia hatima ya kufunguliwa rasmi December 20,2008 tukio la kihistoria hapa Canton Ohio.
Tukio hili la kipekee lilianza kwa kufunguliwa na Mwenyekiti wa muda Bwana Mohammed Sultan kwa kutoa utambulishi wa wanachama wote na pia kutoa historia fupi ya umoja huu tokea kuanzishwa kwake.Pia Mwenyekiti alitoa mafanikio ya mpaka sasa yaliyofikiwa na umoja na jitihada zake zote ambazo zimepelekea kufikia kilele cha kuanzisha umoja huu na matatizo ambayo wameweza kuyapitia kama wana umoja na kuyashughulikia kufikia masuluhisho yake kwa fanaka ya hali ya juu.
Mwenyekiti wa muda alikata utepe kuashiria kuanzishwa kwake rasmi tukio ambalo lilishuhudiwa na wanachama kwa furaha kubwa huku wakiimba wimbo wa Taifa la Tanzania.Pia ilikuwepo keki kubwa ambayo ilikatwa na kulishwa watoto kwa niaba ya wana umoja wote kuashiria tunajenga legacy kwa ajili ya watoto wetu watanzania tuliowapata ugenini kuweza kuja kuendeleza umoja wetu huu.Kama anavyosema Rais mpya wa America "success comes from bottom up" ndio nia yetu tunayolenga ianze kwa watoto wetu kuweza kufikia kufanya ordinary things to extraordinary.
Wanachama walipata fursa pia ya kuongea mengi yanayohusu umoja na kuona picha halisi ya future ya umoja kuanzia 2009 malengo haswa ya umoja kama walivyoyadiscuss katika kikao kilichopita cha Dec wanachama walilenga kufanya mengi makubwa kuliko waliyoyafanya kwa mwaka 2008.
Wana umoja kwa kauli moja walikubaliana mwaka 2009 uwe ni mwaka wa mafanikio na moto zaidi katika kufanikisha malengo ya chama nje na ndani ya chama.Kujenga amani zaidi na kulenga zaidi upendo ndani ya wanachama.Kuongeza idadi ya wanachama iwe kubwa zaidi haswa wadada wetu.
Pia wanachama waliombwa kuhudhuhuria vikao vinavyoitishwa na chama kwa wingi ili kujenga misimamo ya chama kwa pamoja.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

No comments:
Post a Comment